GT Bible Studies    

    Swahili    


Navigation Glad Tidings Bible Studies in Swahili

2. WACHUNGAJI MAKONDENI Luka 2:8-20


TAZAMA: Wakati wa Yesu wachungaji walidharauliwa kwa sababu hawakuweza kutunza sabato. Kwa mfano hawakukubalika kuwa mashahidi katika mahakama. Katika Agano la Kale, malaika waliwatokea watu maalumu kama vile Abrahamu, Ezekieli na Danieli.
1. Fikiria juu maisha ya kila siku ya wachungaji katika milima ya Uyahudi. Walikuwa na furaha zipi na huzuni upi?
  • Je unafikiria nini juu ya uhusiano katik ya wachungaji na Mungu, ambaye amri zake hakuweza kutunza?

    2. Yerusalemu ulikuwa karibu na Bethrehemu, ukiwa na watu wengi waliokaa kule. Kwa nini malaika hawakuwatokea wale watu badala ya wachungaji?
    3. Inasema katika mstari wa 9 malaika walipatwa na hofu kuu. Waliogopa nini?
  • Unaogopa nini siku hizi? (Jibu katika moyo wako.)

    4. Nini kiliwafanya wachungaji kuwa na furaha waliposikia maneno ya malaika (10-12)?
  • Ebu sikiria malaika kusema mstari.10-11 kwako wewe. Je unafikiri ungeweza kuwa na furaha? kwa nini, kwa nini sio?
    5. Wachungaji walifikiria nini waliposikia kuwa mwokozi aliyetarajiwa siku nyingi alikuwa amelala katika hori la ngome? (Hori ni sehemu ambayo ngombe wanakulia nyasi kavu.)

  • Ingesikiaje kama ungeambiwa: "Mwokozi wa ulimwengu amelala katika sufuria ya kuogea?"
    6. Malaika walikuwa na sababu gani kufurahia juu ya kuzaliwa kwa mwanae katikati ya uchafu, baridi maadui na chembechembe cha magonjwa (13-14)?
  • Kwa mwokozi kazaliwa katika hali hii?

    7. Kwa nini Mungu alimwonyesha mtu mwingine mara tu arlipozaliwa?
    8. Malaika waliwezaje kupata hori la ngombe katika ya usiku?
  • Kwa misingi ipi wachungaji waliweza kutambua kuwa motto aliyelala katika hori la ngombe ni Kristo Bwana?

    9. Ni nini kilichokuemo katika maneno ya wachungaji kilichompa faraja Mariamu na Yusufu ambao walikuwa na usiku mgumu?
  • Kwa nini Mungu alituma malaika kwa Mariamu na Yusufu - Kwa nini hatuma wachungaji badala yake?
    10. Wachungaji waliwambia watu juu ya waliyoyaona na kusikia usiku ule wa Kristmas. Kwa nini wengine wote hawakwenda kumsujudu mtoto Yesu?
    11. Ilichukua miaka 30 kabla ya Yesu kuwa maalufubecame - Wachungaji wangi wale walikuwa wamekuwa wakati huo. Maisha ya wachungaji yalibadilikaje baada ya kumwona Mwokozi? Ni nini hakikubadilika?
  • Wachungaji waligundua nini juu ya uhusiano wao na Mungu kupitia kwa matukio haya?
    HABARI NJEMA: Malaika waliimba juu ya amani na furaha usiku ule wa Kristmas. Amani na furaha, hata hivyo, gharama ambayo aliweza kulipa. Alianza kulipa katika hori la ngombe na akamaliza kulipa msalabani.


    ***

    Version for printing    
    Downloads    
    Contact us    
    Webmaster